DAVID MGWASA - TBL
Kutokana na juhudi binafsi za kuipromoti African Stars Band kwa
njia mbalimbali.
TBL
Kampuni iliyochangia kwa kiasi kikubwa kuidhamini African Stars
toka ilivyokuwa changa.
OTHMAN MFURU- BAHARI BEACH HOTEL
Kutokana na juhudi zake binafsi,kwa kuilea African stars tokea
uchanga wake toka ilipoanzishwa july 1994 mpaka sasa.
RADIO
TANZANIA
Redio ya kwanza kuweza kuzipromoti bendi za MK group na MK beats
ambazo ndio chimbuko la African stars. Kazi zote zilizofanywa
na bendi hizo wakati huo zimerithiwa na African Stars Entertainment
ambayo inaendelea kuzisimamia mpaka sasa.
ITV/
RADIO ONE
Moja ya vyombo vya habari vilivyo chini ya IPP limited ambavyo
vimechangia kwa kiasi kikubwa kuipromoti African Stars band na
African Revolution kwa kuweza kupiga muziki na kuwatengenezea
video ambazo huonekana kwenye Televisheni
MWANANCHI/ KITANGOMA
Ni gazeti jipya ambalo nalo liko mstari wa mbele kupromote wasanii
mbalimbali.
JOSEPH KUSAGA - MD CLOUDS ENTERTAINMENT
Kwa juhudi zake binafsi tumekuwa naye kwa karibu zaidi toka enzi
alipokuwa akiendesha Mawingu(Clouds) Disco pale New Africa Hotel
Ghorofa ya Saba wakishirikiana na The Mk Group katika kutoa burdani
hotelini hapo, na mpaka sasa akiwa na Clouds Entertainment amesaidia
sana kwa njia moja au nyingine kuzipromote bendi zetu za African
Stars na African Revolution.
CLOUDS RADIO FM 88.4
Ni redio ambayo inayozipromoti bendi za African Stars, African
Revolution na bendi nyingine za Kitanzania kwa kiasi kikubwa sana.
THE
GUARDIAN Ltd
Ni kampuni inayo miliki magazeti kama vile Nipashe,Alasiri,The
Guardian nk ambayo haiko nyuma pia kupromoti bendi zetu za hapa
nchini bila kusahau African Stars na African Revolution
BUSINESS TIMES Ltd
Ni kampuni inayo miliki magazeti kama vile Majira,Dar leo nk ambayo
haiko nyuma pia kupromoti bendi zetu.
HABARI CORPORATION
Ni kampuni inayo miliki magazeti kama vile Mtanzania,Bingwa,Rai
nk ambayo haiko nyuma pia kupromoti bendi zetu.
UHURU/ MZALENDO
Magazeti ya Uhuru na Mzalendo yameonyesha juhudi zake za kutupromote
tokea enzi za MK group na Mk beats.
DAILY
NEWS
Magazeti ya serikali ambayo yameonyesha juhudi zake vile vile
toka enzi MK group na Mk beats.
DTV/CHANNEL 10
Televisheni zinazopromoti bendi na wasanii wetu katika vipindi
kama vile 'Nani ni nani'
TELEVISHENI YA TAIFA - TVT
Televisheni yenye vipindi vinavyopromoti bendi zetu kama vile
'Usiku wa raha'
SHOGHOLO CHALI -BASATA- SECRETARY GENERAL
Katibu wa Baraza la Sanaa la Taifa kwa kutoa ushauri katika kuzijenga
bendi zetu na kutupa moyo toka enzi za MK group mpaka sasa tukiwa
na African Stars Band na African Revolution Band.
FARAHANI MZEE - CHAMUDATA
Katibu wa CHAMUDATA ambaye ametusaidia kwa kutoa ushauri na miongozo
mbalimbali katika kuzijenga bendi zetu toka enzi za MK group mpaka
sasa tukiwa na African Stars Band na African Revolution Band.
RADIO
UHURU
Kwa kupromoti muziki wetu na bendi zetu za African Stars na African
Revolution
RAILWAY CLUB- SINGA SINGA
Ni klabu ya kwanza iliyotukaribisha katika ukumbi wao na kuweza
kuzitangaza bendi zetu mjini,baada ya kuhama toka mahotelini ambako
tulikuwa tukipiga kama resident bands.
PAPAA
MUDDY
Kwa kutoa mchango wake binafsi katika kuzipromote bendi zetu katika
kumbi mbali mbali na hasa zilipokuwa zikitumbuiza Railway Club
- Singa Singa
MANGO
GARDENS
Sehemu ambayo tumekuwa tukiitumia kama ukumbi wetu wa nyumbani
na ndipo palipo tupo umaarufu tulionao.
CLUB
BILICANAS
Management yao tumekuwa nayo na uhusiano wa karibu katika maswala
ya burudani tukishirikiana toka enzi za MK group mpaka hivi sasa
tukiwa na African Stars kwenye usiku wa mwafrika.
TCC
CLUB
Club ambayo tumekuwa tukishirikiana nayo toka enzi za MK Group,
MK Beats na MK Sounds na mpaka hivi sasa tuko nao pamoja tukiwa
na African Stars - Twanga pepeta katika kutoa burudani kila siku
za jumapili.
MEHBOOB - FKW DISTRIBUTORS
Huyu ni Distributor wetu Amekuwa mstari wa mbele katika usambazaji
wa kanda zetu,(video tapes na audio tapes)
CAP
KOMBA -TOT
Ni mtu ambaye ametoa changamoto(challenge) katika kufanya muziki
wetu uwe wa kiushindani na tunampongeza kwa kuwapeleka wasanii
wake shule ili wajaribu kutukaribia kama siyo kutufikia.
MIRAJI SHAKASHIA - AFRICAN STARS BAND
Huyu ni kijana ambaye tumekuwa naye toka angali mdogo katika enzi
za MK Group akicharaza Solo Guiter na hivi sasa tunaye akicharaza
hilo solo katika Twanga Pepeta.
MSICHOKE KOMBO -AFRICAN REVOLUTION BAND
Huyu naye pia tumekuwa naye akiwa mdogo sana toka enzi za MK Group
wakati huo akilicharaza Bass Guiter na hivi sasa anaendelea kulipiga
hilo Bass kisawasawa katika bendi yetu ya African Revolution -
Tam Tam
VODACOM
Kampuni ambayo imetudhamini katika Uzinduzi wa album yetu ya Chuki
Binafsi na tunatumaini kuendelea kuwa nayo pamoja katika maswala
ya promotion.
PRIDE
COMPUTERS
Kampuni ambayo tumekuwa tukishirikiana nayo kwa karibu zaidi katika
kushughilikia utengenezaji wa kazi zetu (Products) hasa upande
wa graphic na printing works pia kwa kiasi kikubwa wameshughulikia
design ya Website yetu ya mwanzo kabisa
|